Posts

Showing posts from August, 2017

ZITAMBUE DALILI NA ISHARA ZA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI

Upungufu wa damu mwilini huambatana na DALILI zifuatazo ; Kuchoka kirahisi Kushindwa kula na kunywa (hasa kwa watoto) Kizunguzungu na kupumua kwa shida hasa kwa akinamama wajawazito wanapofanya shughuli yoyote Historia ya kula udongo (Hasa kwa watoto na wakina mama wajawazito Ishara zifuatazo huambatana na na upungufu wa damu mwilini Weupe wa viganja, nyayo, chini ya kucha, konjactiva na ulimi Dalili za kushindwa kupumua ( kupepeta kwa pua ,kubonyea kwa kifua wakati wa kuvuta hewa, kupumua kwa shida au kutoa sauti ya kugugumia au miluzi wakati wa kuvuta hewa) Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi kama vile (  Kupumua kwa shida ,mapigo ya moyo kwenda kasi, moyo kudunda hovyo, kuvimba mwili, kuvimba macho na ini kuuma na kuvimba linapotomaswa )

KWA NINI KILA MJAMZITO NI LAZIMA APEWE SP?

Image
SP (SULFADOXINE PYREMETHAMINE ) ni dawa imayotumika kama tiba ya tahadhari kwa vipindi kwa wajawazito. Kwa sasa hakuna dawa ya kinga ya ugonjwa wa malaria (Chemoprophylaxis) kwa wajawazito yenye ufanisi na usalama wa uhakika. Kwa sasa mbinu bora itumikayo ni kuondoa maambukizo ya vimelea vya malaria kwenye kondo la nyuma Maambukizi ya malaria kwenye kondo la nyuma husababisha madhara ya malaria kwenye kipindi cha ujauzito. NINI MADHARA YA MAAMBUKIZI YA MALARIA KWENYE KONDO LA NYUMA? Madhara ya maambukizi ya malaria kwenye kondo la nyuma hutokea kwa mama na kijusi nayo ni Upungufu wa damu kwa mjamzito Mtoto kuzaliwa akiwa na uzito pungufu Kijusi kufa tumboni Kuzaa kabla ya wakati Kijusi kudumaa tumboni Watoto wachanga kuzaliwa wakiwa na malaria Kwa ajili ya kuzuia madhara yatokanayo na malaria katika kipindi chote cha ujauzito, kwa uchache dozi tatu za SP zitatolewa SP HUTOLEWAJE KWA WAJAWAZITO? Kama tiba ya tahadhari kwa vipindi SP hutolewa kwa wajawazito wote kila...

PAMS foundation co-founder shot dead in Dar-es-salaam

Dar es Salaam, Tanzania We are heartbroken to share the news that PAMS Foundation co-founder, Wayne Lotter was shot and killed last night in the Masaki District of Dar es Salaam, Tanzania. Wayne devoted his life to Africa’s wildlife, from working as a ranger in his native South Africa as a young man to leading the charge against poaching in Tanzania. Wayne cared deeply about the people and animals that populate this world. In 2009, he teamed up with Krissie Clark and Ally Namangaya to form the PAMS Foundation. Together they worked tirelessly with communities in Tanzania to protect the country’s wildlife. Wayne believed communities were the best protectors of the continent’s animals. Through his work with PAMS he helped train thousands of village game scouts in every corner of the country. His ground-breaking work in developing an intelligence-based approach to anti-poaching helped successfully reverse the rampant rates of poaching facing Tanzania. Wayne’s cha...

UTI (URINARY TRACT INFECTION) NI NINI ?

Image
UTI ni maambukizi kwenye njia ya mkojo kitaalam tunaita Urinary Tract Infection. Kama wewe ni mwanamke uwezekano wa kupata maambukizi haya ni mkubwa kwa sababu za kimaumbile. SABABU ZA UTI KWA WANAWAKE Kwa wanawake njia ya mkojo (urethra) ipo karibu na njia ya haja kubwa hivyo wadudu aina ya bacteria kama E.coli wanaweza kusafiri kirahisi kutoka njia ya haja kubwa na kuingia njia ya mkojo na kusababisha maambukizi maana kwa kawaida wadudu hawa husafiri mpaka kwenye kibofu. na ndio maana baada ya kutumia maliwato wananwake hushauriwa kujifuta kutoka mbele kuelekea nyuuma kupunguza uwezekano wa maambukizi haya NINI DALILI ZA UTI ? Maumivu wakati wa kukojoa Hali ya kutaka kukojoa mara kwa mara japo mkojo hutoka kidogo Maumivu ya mgongo na sehemu ya chini ya tumbo Mkojo mchafu na wenye harufu isiyo ya kawaida Kujisikia mchovu na homa UCHUNGUZI Unapohisi dalili hizi wahi hospitali ambako utaombwa utoe mkojo utakao fanyiwa uchunguzi ili kubaini uwepo wa wadudu wanaosababis...