ZITAMBUE DALILI NA ISHARA ZA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI

Upungufu wa damu mwilini huambatana na DALILI zifuatazo ;
  • Kuchoka kirahisi
  • Kushindwa kula na kunywa (hasa kwa watoto)
  • Kizunguzungu na kupumua kwa shida hasa kwa akinamama wajawazito wanapofanya shughuli yoyote
  • Historia ya kula udongo (Hasa kwa watoto na wakina mama wajawazito
Ishara zifuatazo huambatana na na upungufu wa damu mwilini
  • Weupe wa viganja, nyayo, chini ya kucha, konjactiva na ulimi
  • Dalili za kushindwa kupumua ( kupepeta kwa pua ,kubonyea kwa kifua wakati wa kuvuta hewa, kupumua kwa shida au kutoa sauti ya kugugumia au miluzi wakati wa kuvuta hewa)
  • Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi kama vile (  Kupumua kwa shida ,mapigo ya moyo kwenda kasi, moyo kudunda hovyo, kuvimba mwili, kuvimba macho na ini kuuma na kuvimba linapotomaswa )

Comments

Popular posts from this blog

KWA NINI KILA MJAMZITO NI LAZIMA APEWE SP?

ARTESUNATE TIBA SAHIHI KWA MALARIA KALI