ARTESUNATE TIBA SAHIHI KWA MALARIA KALI

MALARIA NI NINI?
Malaria ni ugonjwa unaosababishwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo plasmodia.
Ugonjwa huu husambazwa na mbu
NINI DAWA YA MALARIA ISIYO KALI
Malaria isiyo kali hutibiwa kwa dawa mseto maarufu kama Artemether lumefantrine (ALU)
ZIPI NI DALILI ZA MALARTIA KALI?

  • Kulegea kupita kiasi
  • Mabadiliko ya tabia kama vile maluweluwe, kuhisi au kuona vitu visivyo kuwepo
  • Kupumkua kwa shida
  • Manjano
  • Kutapika kila kitu
  • Kushindwa kula au kunyonya
  • Damu kushindwa kuzunguka mwilini
  • Kutokwa damu kirahisi na mara kwa mara

NINI TIBA SAHIHI YA MALARIA KALI
Dawa ya sindano iitwayo Artesunate ndio dawa chaguo la kwanza katika kutibu malaria
Dawa hii huweza kutolewa kwa njia ya mshipa au msuli kwa kipindi kisichopungua masaa 24
Baada ya hapo matgibabu hukamilishwa kwa kumpatia mgonjwa dozi kamili ya ALU
HAISHAURIWI  kutumia artesunate kwa wajawazito wenye mimba iliyo na umri chini ya miezi mitatu
DAWA YA KWININI ITUMIKE KWA WAJAWAZITO WENYE MIMBA YENYE UMRI CHINI YA WIKI 12 NA KWA WALE WENYE MZIO (ALLERGY) NA ARTESUNATE

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

KWA NINI KILA MJAMZITO NI LAZIMA APEWE SP?

ZITAMBUE DALILI NA ISHARA ZA UPUNGUFU WA DAMU MWILINI